Imaam Al-Albanee Kuhusu Jihaad
Imetayarishwa Na: Imaam Muhammad Nassir-ud-Deen al-Albanee
Asili: Kanda za tepu, "Fataawa hawl al-Jihaad al-afghaani", na "shubuhaat mud'iyeel Jihaad."
Imefasiriwa Na: Abu-Farida Muhammad Awadh Basawad

Bismillaahir Rahmaanir Raheem

Ifuatayo ni tafsiri kutoka katika  'Fataawaa al-Albaanee (baadhi ya kandaa za tepu zilizonukuliwa za Shaykh) wakati shaykh alipoulizwa rai yake kuhusu Jihaad.

Bayana kwa mukhtasar:

Ndugu zangu wapendwa waume kwa wake ningelipenda kuidhihirisha bayana ya fatwa ifuatayo ya Shaykh wetu mpendwa, Shaykh Muhammad Naasir ud-Deen Al-Albaani (rahimahullaah)...

Asli yake ilipatikana kutoka katika kanda ya tepu ya darasa ya Shaykh Al-Albaani, ambamo ndani yake aliulizwa suali kuhusiana na matayarisho ya kujiandaa kwa Jihaad ya kufanya mashambulizi; ambapo Waislamu wanapotakiwa kutoka katika miji yao ya kiislamu ili kupigana vita na Makuffaar, kinyume cha Jihaad ya ki-leo ya kujihami; ambapo miji ya kiislamu imevamiwa na kushambuliwa na Makuffaar, kwenye hali zote hizo - kama alivyoeleza waziwazi Shaykh - vita hivyo vyao vinakuwa ni Fard 'ayn juu ya Waislamu (yaani: waajib unaompasa kila mwenye uwezo).

Inaonekana yakwamba kiini cha suala hilo, au malengo ya mjadala kuhusu Fatwa hii - ambao ungelikuwa ni wenye kuondoa shaka katika suala hili - kwa sababu fulani ukawachwa bila ya mazingatio yoyote...

Na kwa hakika, matokeo ya kutoelewa vyema, au kufahamu vibaya huko kwa ajili ya ukosefu huu ni bahati mbaya... Kwa sababu Fatwa hii imetapakaa katika mitandao, na kawaida hufuatana na madai ya urongo yasemayo eti uimarishaji wa Jihaad siku hizi na zama hizi zetu - iwapo ni wa Kuvamia, au Kujihami - haijuzu pasi na kuwepo Khaleefah, au Imaam kwa Waislamu wote.

Lakini madai haya ni ya uwongo, na upuzi. Kwani yoyote mwenye kufanya utafiti wa zama za kina Tatar (kina Mongol) - ambao waliotangazwa kuwa ni Makuffaar na Ma 'Ulamaa - Waliiuwa Khilaafah ya Waislamu, kisha wakajichagulia wenyewe utawala wa Ulimwengu wa Kiislamu, mtu atajionea, bi-idhnillaah, yakwamba - hatakama hapakuwepo na Khilaafah - Waislamu wakaingia vitani na kupigana Jihaad, wakawauwa  na kuwatenza nguvu Makuffaar, hivyobasi kui-imarisha tena Khilaafah kwa mara nyengine tena - na miongoni mwao akiwemo Ibn Taymiyyah (rahimahullaah) mwenyewe!

Kwahivyo, haya madai ya kuhusu Jihaad ya kujihami, ni ya urongo.
Vilevile inajulikana, kama ilivyoelezwa katika Fatwa hii, yakwamba Shaykh Al-Albaani Allaah (Ta'aala) Alija'alie kaburi lake ling'are) anaamini yakwamba Jihaad ya huko Afghanistan ilikuwa ni Jihaad iliyosihi - na pia, ni jambo la dhahiri, hapakuwepo Khilaafah, au Ameer kwa Waislamu wote waliokuweko wakati huwo... sasa hali hii ya urongo ilitoka wapi?... Haikutoka kwa Ma'ulamaa wa kikweli.

Mtu akiwa na ikhlasi katika kuutafuta ukweli wa mas-ala haya, basi namnasihi kila mmoja ajipatie baadhi ya darsa za Shaykh Al-Albaani kuhusu Jihaad, ambapo ameeleza msimamo wake waziwazi kuhusu aina mbili za Jihaad - Jihaad ya Uvamizi na Jihaad ya Kujihami.

Kwa mfano, katika kanda yake ya tepu "Fataawa hawl al-Jihaad al-afghaani."[1] mwanafunzi mmoja alimuuliza iwapo Jihaad ya Afghanistan ni Fard 'ayn, au Fard kifaayah, na Shaykh akajibu yakwamba ni Fard 'ayn, kwa sababu idadi ya Waislamu wanaopigana na jeshi la Mushrikeen la Urusi (Russia) halikuwa la kutosha. Pia akasema yakwamba kila Muislamu ilimpasa ashiriki kwenye Jihaad hii...

: Waislamu wanapigana kwa ajili ya kulienua neno la Allaah (Ta'aala), na/au kuzilinda ardhi zao Kuhusu suala la Jihaad ya Uvamizi (ambayo inayofuata), basi namnasihi kila mmoja aisikilize tepu ya Shaykh,  "Shubuhaat mud'iyee al-Jihaad." Katika darsa hii akaubainisha msimamo wake kuhusu kujiandaa kwa Jihaad ya Uvamizi, na ni aina hii ya Jihaad ambayo - kulingana na maoni ya Shaykh - inaweza kutekelezwa chini ya Ukhalifa, na hii Jihaad ya Kujihami (yaanikutoka kwa Makuffaar) inaweza kutekelezwa chini ya Ameer,  au bila ya Ameer wa Waislamu wote...

Na hii ndiyo misemo ya Ma'ulamaa.
Na asili ya kila uongofu unatoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aala).
Abu Suhayb


Jawabu:

"Kuhusu Jihaad, Ewe ndugu yangu, katika wakati huu na kabla ya wakati huu, ni fard 'ayn, kwa sababu matatizo tuliyo nayo si matatizo ya Bosnia na Chechnya (peke yao) amabyo yamewaathiri vijana wengi na kuwatia hamasa. Kwani hapa jiranini mwetu, kuna Mayahudi ambao walioivamia Falesteen, na hata nchi moja ya Kiislamu haijajisongeza kutekeleza wajibu wa kupambana nao Jihaad, na kuwang'oa na kuwatumbukiza  baharini, kama walivyosema baadhi au mmoja wa Ma-Rais wa nchi za Kiislamu.

Na nukta iliyoko hapa ni kwamba Jihaad ni fard ayn, kwa sababu nchi nyingi za Kiislamu zilivamiwa zamani mpaka hivi sasa na Makuffaar. Na mifano ya Uvamizi huwo haikufichika kwa Muislamu mwenye kujishughulisha na harakati za waislamu, bila ya kuvitaja vikundi vya Kiislamu au vipote vya Kiislamu au nchi za Kiislamu.

Lakini Jihaad ina nguzo na sheria zake, na sisi - kikundi cha wanavyuoni wa Kiislamu - tunaamini yakwamba Jihaad ya faradhi itawalazimu peke yake waislamu ambao watakaosaidiana katika kusimamisha yale yaliyoamrishwa juu yao kutoka katika Jihaad dhidi ya makuffaar, na kuwang'oa kutoka katika ardhi au nchi walizozivamia.

Na kwa sasa hatuhitaji kuleta ushahidi kutoka katika Kitaab na Sunnah, kwani nukta hii imeafikiwa na wanavyuoni wote - yakwamba Jihaad ni  fard ayn ikiwa sehemu ya ardhi ya waislamu imevamiwa, sasa itakuwaje iwapo uvamizi huwo umetokea kwenye ardhi nyingi.?!

Lakini, kwa bahati mbaya napenda kusema yakwamba Jihaad hii ambayo ni fard - bali ni fard ayn - si kitu kinachowezekana kutekelezwa na watu binafsi kama ilivyokuja kwenye suali lenyewe, bali hata na baadhi ya makundi ya kiislamu. Kwa sababu mifano ya Jihaad kama hii, haswa katika hizi zama zetu ambazo uwezo wa ki-vita umekuwa mwingi, haiwezekani  kutekelezwa na vikundi vya kiislamu na watu binasfi ndio hata usiwataje! Lakini wajibu ni juu ya hizi Serikali, na zile nchi za kiislamu ambazo zilizo na uwezo wa kujitayarisha kwa vita,  na, na uwezo wa vita vya kisasa, ambao watakaposhirikiana kwa ikhlaas kwa Jihaad hii, basi watakuwa ni wenye kuitekeleza fard ayn. Lakini, kwa masikitiko makubwa, nchi hizi hata hazijatukusa viungo vyao katika kulitekeleza jambo hilo.

Kwahivyo, pengine wanalihusisha suala hilo la Jihaad na makundi na mapote mbalimbali ya Uislamu, ambapo haya hayana uwezo wowote wa kuzuiya kuingiliwa /uvamizi wa Makuffaar. Na matukio ya kilimwengu yameshuhudilia uhakika yakwamba kila kikundi cha Kiislamu kinachojaribu, emma kupambana na adui kwa mfano kama ilivyotokea huko Afghanistan, au kwa kufanya uasi dhidi ya kiongozi ambae Ukafiri wake umedhihiri, kwa mfano, kama huko Algeria - kisha matukio haya ya bahati mbaya yanaonyesha kuwa Jihaad ya watu binafsi au Jihaad ya kikundi haileti matunda yanayotarajiwa, nalo ni kwamba Neno la Allaah lifanywe kuwa bora kuliko chochote.

Sasa kwahivyo, tunaamini yakwamba Jihaad hii haiwezekani isipokuwa kwanza iwe chini ya mamlaka ya Kiislamu, na chini ya kikundi cha Kiislamu chenye watu kutoka katika nchi mbalimbali, badala ya wote kutoka katika nchi moja au sehemu moja.

Na juu ya hayo kupatikane umuhimu wa Taqwaa ya Allaah, kwa kujiepusha na yale ambayo Allaah aliyoyaharamisha kutoka katika mambo ya kawaida yanayojulikana sana miongoni mwa Waislamu, lakini kwa masikitiko makubwa wao wako mbali sana na kuyatekeleza  hayo.
Na pia tumetaja - na najaribu kuyafupisha maneno yangu kadiri ya uwezekano uliopo - mara nyingi yale yanayowasibu waislamu leo, huu utwevu na udhalilifu/fedheha mambo ambayo hayakuwa ni yenye kujulikana kabisa katika tareekh (historia) ya Kiislamu, ni kwamba Waislamu hawakuweza kutekeleza, kwa uchache, hata aya moja ya Qur'aan... na hayo ni maneno ya Allaah (kama yalivyofasiriwa):

"Enyi mlioamini! Mkiinusuru dini ya Allaah, naye Atakunusuruni na Ataithubutisha miguu yenu". [Soorah Muhammad 47:7]

Hapana shaka yoyote yakwamba nusra hii ya waislamu kutoka kwa Allaah, ni nusra ya kuibainisha Hukmu ya ki-Sheriya ikawa ni ukweli wenye kutekelezwa, na kwa bahati mbaya jambo hili halizingatiwi katika nchi nyingi za Kiislamu, au hata kwa waislamu wenyewe nafsi zao. Na miongoni mwa hizo nchi za Kiislamu zenye baadhi ya chembe-chembe za hukmu kulingana na Sheriya ya Allaah hazijaweza, mpaka sasa kupiga mbiu ya mwito wa Jihaad.

Na kutokana na hayo waislamu na mataifa watabakia dhaifu maadamu haijatokea nchi  yoyote ya kiislamu iliyoienua bendera ya Jihaad, na Jihaad hiyo ambayo inayoitisha mapambano dhidi ya wale walio karibu nao, sio wale walio katika upeo wa mbali na wao. Kwa waislamu, pamoja na nchi zao, na makundi yao, na vipote, na kwa watu binafsi, iwapo hawatoweza kupigana Jihaad na wale waliopakana nao au walio karibu nao basi hawatoweza kupigana Jihaad na wale walio mbali nao... kwa mfano Eritrea, Somalia, Bosnia na Chechnya.

Sasa tutayataja kutokana na haya, majukumu juu ya vijana wa Kiislamu kila mmoja kwa nafsi yake na kwa makundi na kwa mapote yakwamba kwanza wausambaze ujumbe wa Uislamu kwenye nchi, na pili ni kwa viongozi - na ufahamu huwo (wa kisawasawa) uambatane na watu wote hao wahukumiane kulingana na yale yaliyoteremshwa na Allaah.

Kiongozi anatakiwa atawale kulingana na yale yaliyoteremshwa na kuamrishwa katika Kitabu cha Allaah. Na kila mtu kwa nafsi yake ahukumu kulingana na yale yaliyoteremshwa na kuamrishwa katika Kitabu cha Allaah... Najua mimi leo vijana wengi, na makundi na mapote, huwasukumizia majukumu hayo (mambo ya kilimwengu) viongozi peke yao, haliyakuwa imethubutu katika imani yangu yakwamba majukumu ni yenye kumkabili kila mtu, makundi na mapote, kama yanavyowakabili viongozi hawa! Hii ni kwa sababu serikali hizi zimesimamishwa kutoka katika ardhi za waislamu...waislamu hawa ambao waliolinganiwa kwa hadeeth mbili kutoka kwa Mtume (Sallallaahu 'alayhi wasallam)... ya kwanza ni maneno yake (Sallallaahu 'alayhi wasallam) aliposema:

'Mutakapo jishughulisha na biashara za riba na kushikamana na mikiya ya ng'ombe, na mukaridhika na mambo ya ukulima (mashamba) na mukawachana na kupigana jihaad kwa ajili ya Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wata'aalah), basi Mwenyezi Mungu atawadhalilisha. Na hatowaondolea udhalilifu huo mpaka muregee kwenye dini yenu'".

Na hadeeth nyengine ni maneno yake (Sallallaahu 'alayhi wasallam) aliposema:

"Hivi karibuni mataifa yataitana kuungana dhidi yenu, kama vile watu wanavyoitana kuja kula kutoka kwenye sinia ya chakula."

Akauliza mtu mmoja: "Litakuwa jambo hilo kwa ajili ya idadi yetu itakavyokuwa chache, Ewe Rasoolullaah (Sallallaahu 'alayhi wasallam)?"

Akajibu Mtume (Sallallaahu 'alayhi wasallam): "Laa, mutakuwa idadi yenu ni kubwa, lakini mutakuwa ghuthaa'a kama zile takataka za povu zinazo-olea juu ya kidimbwi cha maji, na Allaah (Subhaanahu wata'aalah) ataondoa khofu kutoka katika nyoyo za maadui zenu (ya kuwaogopa nyinyi) na atawaekea kwenye nyoyo zenu WAHN."

Wale waliokuwepo pale wakauliza: "Na ni nini hiyo WAHN, ewe Rasoolullaah (Sallallaahu 'alayhi wasallam)?"

Akajibu Mtume (Sallallaahu 'alayhi wasallam): "Ni kuyapenda maisha ya kidunia na kuyachukia mauti.

Na matukioa kama haya yaliyotajwa na Mtume (Sallallaahu 'alayhi wasallam) katika hadeeth hii sasa yametokea katika jamii zote za waislamu, na ni miongoni mwa dhulma zilizodhahiri  zenye kuupalilia ukandamizaji huu kwa  waislamu mpaka nyoyo za viongozi, na watu binafsi zikafunikwa zote na weusi (kutokana na madhambi yao).

Miji ya Kiislamu haihukumiani kwa yale yaliyoteremshwa na Allaah, na lau kama kuna mji mmoja miongoni mwao ambao (unaodai) kuhukumu kwa yale yaliyoteremshwa na Allaah, basi ishara ya kwanza iliyo wazi yenye kuonyesha yakwamba haihukumiani kwa yale yaliyoteremshwa na Allaah ni kwamba hawaupaazi mwito wa Jihaad.

Sasa ikiwa wakati huu sio wakati ambao Jihaad katika njia ya Allaah haiwezekani kuwa waajib, na miji mengi ya kiislamu imeshavamiwa, basi ni lini hapo Jihaad itakapokuwa wajibu?

Lakini tatizo ni kwamba - na huu ndio moyo wa suala zima - ni kwamba hakuna yoyote miongoni mwetu mwenye uwezo wa kuiendeleza (Jihaad hii), kwanini?... Kwa sababu sisi twazama ndani ya madhambi, na twazama ndani ya ikhtilafu za vipote na ikhtilafu za kitaifa , na sisi twajua yakwamba mlango mmoja unaoelekeza kwenye udhaifu na kushindwa ni kukhitalifiana miongoni mwa waislamu wenyewe.

Na hivi karibuni tulifikwa na mtihani wenye kusikitisha sana, nao ni Jihaad ya Afghani, ambapo tulikuwa tukitarajia yakwamba hatima yake itakuwa ni ushindi kwa waislamu, na kukawa na alama madhubuti za kupanda mbegu ya Taifa la Kiislamu. Kisha mwishoe na matokeo yake yakageuka na kuwa kinyume kabisa (cha vile kulivyotarajiwa) kutokana na alama za ushindi wa mapema juu ya adui,  wa-communisti (shuyuiyyeen), walififia wakati tafauti baina ya makabila zikawafanya wagawanyike kwa makundi saba, na Uislamu wao walioufanya kuwa ndiyo Deen haukuwazuiya kufanya hivyo, na Mola wetu akasema (kama ilivyofasiriwa):

"...wala msiwe katika washirikina. Katika wale walioitenga dini yao na wakawa makundi makundi; kila kikundi kinamfurahia kilicho nacho." [Soorah Ar-Rum 30:31-32]

Kwahivyo, ni juu ya yule mwenye kupenda kuhudhuria Jihaad ajiandae vilivyo kwa Jihaad, na maandalizi ya kupata ushindi, na kwa bahati mbaya jambo hilo halizingatiwi katika zama zetu hizi. Na Allaah (Subhaanahu wata'aalah) Amesema katika Qur'aan Tukufu, (kama ilivyofasiriwa):

"Hakika Mwenyezi Mungu habadili yaliyoko kwa watu mpaka wabadili wao yaliyomo katika nafsi zao." [Soorah Ar-Ra'd 13:11]

Kwahivyo, tunamtaka kila muislamu, kila kikundi na kila kipote, wasizizungumze Serikali zenye kujishughulisha kuusambaza Uislamu uliotahirika na ulio saheeh, uliotahirika kutokana na kila jambo la urongo lililoingizwa ndani yake kwenye zama tafauti, na kisha kuwalea Waislamu juu ya Uislamu huu ulio safi.

Siku ambayo alama hizi zitakapoanza, na zikawa zadhihirika katika ardhi hii pana ya Kiislamu, basi siku hiyo ndiyo zile alama za kuwa tayari kuithibitisha Jihaad ya Fard ayn itakapoanza. Hawa watu wenye kutaharuki wanaokwenda katika nchi nyingi za Kiislamu zilizovamiwa/zilizoshambuliwa na Makuffaar kama vile Bosnia na Chechnya kwa mfano... ni silaha gani walizonazo wao? ni kina nani viongozi ambao wenye uwezo wa kuwasimamia na kuwaongoza na kuwapa maamrisho ya kupigana chini ya mamlaka na chini ya bendera moja? Kwahivyo kama kungelipatikana mamlaka ya aina moja peke yake basi tungeliyaona (matunda) ya Jihaad kama tulivyoyaona  huko Afghanistan (yaani: ushindi juu ya adui). Kwahivyo, Allaah (Subhaanahu wata'aalah) Amesema katika Qur'aan Tukufu, (kama ilivyofasiriwa):

"Basi waandalieni nguvu mziwezao,  na mafarasi yaliyofungwa, tayari tayari, ili kwazo (nguvu hizi) muogopeshe maadui wa Mwenyezi Mungu na maadui zenu." [Soorah al-Anfaal, Aayah 8:60]

Yako wapi matayarisho hayo?! Na ni yupi mwenye uwezo wa matayarisho hayo? Kila mtu kipekee?! Laa, Ni Serikali?...naam ni Serikali, na tunaweza sisi kusema yakwamba michango yao ya matayarisho hayo si midogo...lakini matayarisho haya yamepatikana kutoka kwa maadui zao... sasa ikisimama Jihaad baina ya Waislamu na Ma-kuffaar, mara tu hawa waislamu hawatokuwa na uwezo wa kuwafikishia mahitaji ya silaha majeshi yao isipokuwa kwa kununua kutoka kwa maadui zao.

Sasa kwaweza kupatikana ushindi na Jihaad kwa kununua silaha kutoka kwa maadui wa waislamu?!

Haiwezekani namna hii, na kwa ajili hiyo, matayarisho haya yanatuamrisha sisi, hayawezi kuimarishwa hata na nchi za Kiislamu, kwa sababu nchi za Kiislamu zenyewe hununua silaha zao za maangamizi kutoka kwa maadui zao na mataifa yenye ukandamizaji. Na kuna njia ya kuzitia ganzi silaha hizi (zisiweze kutumika) wakati wao (waislamu) watakapodhamiria kuzitumia dhidi ya jeshi la makafiri. Na kwa ajili hii, mimi nasema, na namalizia maneno yangu na jawabu langu kwa suala hili yakwamba pindi Allaah Aliposema (kama ilivyofasiriwa):

"Basi waandalieni nguvu mziwezao..."

Tangazo hili lilikuwa ni kwa Maswahaba wa Mtume (Sallallaahu 'alayhi wasallam), kisha tangazo hilo likawa ni kwa mujtama' mzima wa waislamu kwa kutokana na ujumla wa maandishi yenyewe. Lakini tangazo hili liliwaelekea Maswahaba baada yakwamba wamelelewa juu ya malezi ya Uislamu saheeh mpaka wakawa na uwezo wa kuimarisha mfano wa tangazo hilo - kutayarisha nguvu za kilimwengu baada ya kutayarisha nguvu za kiroho ndani ya nafsi zao au baina yao wenyewe, kutokana na malezi waliyokulia nayo kutoka kwa Mtume wao (Sallallaahu 'alayhi wasallam).

Na taarekh (historia) hujirudia yenyewe...Sasa inatakikaniwa kupatikane malezi ya taifa kutoka katika Mataifa ya Kiislamu ili kuwe na uwezekano wa taifa hilo kuimarisha haya mambo ya matayarisho ya kilimwengu, na sisi leo hatuoni taifa lililoimarisha wajibu huu ambao tunaweza kuufafanua kwa maneno mawili: tasfiyyah na tarbiyyah.

(Bali) twajiona kama watu walio tapakaa kila mmoja na nafsi yake. Na lau kama pangelikuwa na kikundi, na juu ya kikundi hichi kuwe na kiongozi mwenye kufanyiwa utiifu na waislamu wote, na akainyanyua bendera ya Jihaad dhidi ya maadui: Jambo hili bado halijawahi kutokea, na kwa ajili hii tunaitisha kuwepo kwa utangulizi/matayarisho ya hii Jihaad Tukufu.

Amma kuhusu kuwa na pupa (kwa hawa watu) na hamasa ingawaje hata hiyo Jihaad ya nafsi haijaonekana kwao - na huwo ndiwo ufahamu saheeh wa Kiislamu, na kuutekeleza kwa ushirikiano, na kwamba aweko juu yao kiongozi baada ya hayo, ambae atakaewahimiza wajiandae kwa nguvu waziwezao na silaha: Kwahivyo siku tutakapo-ona mambo mfano wa hayo, siku hiyo waislamu watakuwa ni wenye kuushangilia ushindi wa Allaah, na Allaah humsaidia amtakae. Hili ndilo jawabu langu la suali lako."


Nukta ya maelezo:
1.Kanda hizi za tepu, "Fataawa hawl al-Jihaad al-afghaani", na "shubuhaat mud'iyeel Jihaad. Alhamdulillaah, nilipata habari kuzihusu kanda hizi, ukiwemo na ubainifu wa kihakika wa Shaykh Al-Albaani kuhusu mas-ala haya, kutoka kwa ndugu mwema ambae ninaemuamini, Tunamuomba Allaah ( Subhaanahu wata'aalah) amjazi kheri.
Allaah ( Subhaanahu wata'aalah) Awasamehe wale wote ambao waliokuwa wameizuiya kanda hii, mpaka sasa, dhana ya urongo iliyoenezwa na yenye kumuhusu Shaykh wetu mpendwa Shaykh Muhammad Naasir ud-Deen Al-Albaani (rahimahullaah) kuhusu suala la Jihaad na hukmu zake. Kwa hakika, yeye -  (Al-Albaani) ameepukana na wale waliomsingizia urongo huu.